pmbet

Iran yawasili Pakistan kwa mazungumzo ya amani na marekani

Eric Buyanza

April 25, 2026
Share :

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amewasili Islamabad, Pakistan kwa mazungumzo yanayolenga kufufua juhudi za amani kati ya Iran na Marekani baada ya wiki nane za mvutano mkubwa wa kijeshi.
 

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema Iran inatarajiwa kuwasilisha mapendekezo yanayoweza kukidhi matakwa ya Washington, ingawa hakufafanua maelezo ya mapendekezo hayo.
 

Hata hivyo, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran amesema hakuna mipango ya mazungumzo ya moja kwa moja kati ya pande hizo mbili, akibainisha kuwa ujumbe wa Iran utawasilishwa kupitia Pakistan.

 

Wakati huo huo, wajumbe maalum wa Marekani, Steve Witkoff na Jared Kushner, wanatarajiwa kuwasili Pakistan kwa mazungumzo hayo, huku Ikulu ya White House ikisema Washington iko tayari kutoa nafasi kwa diplomasia.

 

Mvutano kati ya Iran na Marekani umeendelea kuathiri masoko ya dunia, hasa baada ya Marekani kufanya mashambulizi ya anga na Iran kuzuia njia muhimu ya usafirishaji mafuta ya Strait of Hormuz, hatua iliyochangia kupanda kwa bei ya mafuta duniani.

 

Pande zote mbili zinaonekana kutafuta njia ya kusitisha mgogoro huo, ingawa bado kuna kauli zinazokinzana kuhusu uwezekano wa kufikiwa kwa makubaliano.
 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet