pmbet

Israel yathibitisha kupata maafa makubwa kutokana na mashambulio ya Iran

Eric Buyanza

March 24, 2026
Share :

Jeshi la Israel limethibitisha kuwa shambulio la makombora kutoka Iran limesababisha uharibifu mkubwa katika maeneo ya kati ya nchi, huku vikosi vya dharura na wahudumu wa misaada wakitumwa haraka katika maeneo yaliyoathirika.

 

Picha zilizochapishwa kupitia ukurasa wa Telegram wa huduma za dharura za Israel zinaonesha moshi mzito ukifuka kutoka kwenye majengo, pamoja na vifusi vilivyotapakaa katika eneo lilolengwa na shambulio hilo.

 

Awali, iliripotiwa kuwa kufuatia tahadhari iliyotolewa na jeshi la Israel kuhusu makombora yaliyofyatuliwa na Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi ya Iran (IRGC), wahudumu wa misaada walielekezwa kusini mwa nchi, ambako kulishuhudiwa uharibifu mkubwa kufuatia mashambulizi ya Iran dhidi ya Israel.

 

Katika siku za karibuni, picha zimekuwa zikisambaa zikionesha kiwango kikubwa cha uharibifu nchini Israel.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet