Jamie Carragher Akubali muziki wa Florian Wirtz.
Joyce Shedrack
February 3, 2026
Share :
Jamie Carragher amebadilisha msimamo wake kuhusu ukosoaji wake dhidi ya Florian Wirtz, akisisitiza kwamba kiungo huyo wa Liverpool ni mchezaji maalum miezi michache tu baada ya kumtilia shaka Mjerumani huyo.

Wirtz alianza maisha yake polepole Liverpool baada ya uhamisho wake wa pauni milioni 116, ambazo ni sawa na zaidi ya Shilingi Bilioni 300 za Kitanzania msimu huu wa joto, bila kufunga bao au kutoa pasi katika Ligi Kuu hadi mwanzoni mwa Desemba, lakini sasa ameanza kuonyesha mambo mazuri.
Sasa amefunga mabao manne katika mechi zake saba za mwisho za ligi, huku pia akifunga dhidi ya Qarabag katika Ligi ya Mabingwa wiki iliyopita.
Ligi Kuu imempoteza Kevin De Bruyne, (lakini) tumempata Wirtz. Tunazungumzia wachezaji maalum wanaoingia kwenye ligi yetu. Nimemtazama sana na kufikiria kama anaweza kufikia kiwango cha De Bruyne.
Ninapomtazama Wirtz, nadhani anaweza kuwa mzuri kama David Silva, lakini ana karibu wote wawili.Alisema Mlinzi huyo wa kati wa zamani wa Majogoo.





