Je wajua? Papa Francis aliwahi kuwa Baunsa kwenye Night Clubs
Sisti Herman
April 22, 2025
Share :
Je Wajua?
Kwa mujibu wa historia ya maisha yake, kabla ya kuwa Papa, Francis (Jorge Mario Bergoglio) alisoma somo la kemia na kupata diploma ya fundi wa kemia kutoka shule ya sekondari ya kiufundi. Baadaye alifanya kazi kwa muda mfupi katika maabara ya sayansi ya chakula.
Pia alifanya kazi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kufanya kazi kama msafishaji na mlinzi wa klabu ya usiku wakati wa miaka yake ya mapema.
Papa Francis alifariki dunia jana Aprili 21, 2025, akiwa na umri wa miaka 88, katika makazi yake mjini Vatican, Domus Sanctae Marthae, saa 7:35 asubuhi, kufuatia kiharusi kilichosababisha kushindwa kufanya kazi kwa moyo.