pmbet

Jeshi la Israel lawataka wakazi wa mji wa Gaza kuondoka

Eric Buyanza

September 6, 2025
Share :

Jeshi la Israeli limewataka Wapalestina katika mji wa Gaza kuondoka kuelekea kusini, huku wakionya kuwa jeshi hilo litakuwa na kazi katika mji huo. 

Majeshi ya Israel yamekuwa yakifanya mashambulizi katika viunga vya mji huo wa kaskazini kwa wiki kadhaa baada ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuamuru jeshi kuuteka. 

Netanyahu anasema Mji wa Gaza ni ngome ya Hamas na kuuteka ni muhimu ili kuwashinda wapiganaji wa Kiislamu wa Palestina, ambao mashambulizi yao ya Oktoba 2023 dhidi ya Israel yalizua vita.

Shambulio hilo linatishia kuwafurusha mamia kwa maelfu ya Wapalestina wanaojihifadhi huko kutokana na mapigano ya takriban miaka miwili. Kabla ya vita, karibu watu milioni moja, karibu nusu ya wakazi wa Gaza, waliishi katika mji huo. 

Msemaji wa jeshi la Israel Avichay Adraee aliandika kwenye mtandao X kwamba wakaazi wanapaswa kuondoka katika mji huo kuelekea eneo lililotengwa la pwani la Khan Younis kusini mwa Gaza, na kuwahakikishia wale wanaoondoka kwamba wataweza kupata chakula, matibabu na makazi huko waendako. 

Siku ya Alhamisi, jeshi lilisema lilikuwa na udhibiti wa karibu nusu ya mji. Inasema inadhibiti takriban 75% ya Gaza yote.

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet