Joel Lwaga awafikia wanaoteswa na Mapenzi.
Joyce Shedrack
February 3, 2026
Share :
Mwimbaji wa Nyimbo za Injili Joel Lwaga, katika mwezi wa mapenzi unaojulikana na wengi kama mwezi wa upendo, ameamua kuwafariji watu wanaopitia changamoto za kimahusiano kwa sasa.
Hatua hiyo imekuja sambamba na ujumbe aliouambatanisha kwenye wimbo wake mpya uitwao New Beginning, ambapo amewalenga hasa wale wanaopitia mahusiano yenye sumu (toxic relationships).
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Joel Lwaga amesema:
"Kwa yeyote anayepitia toxic relationship, ninakuombea mwanzo mpya katika Jina la Yesu. Hustahili mateso hayo. Simama, jiondoe katika hali hiyo. Mwenza sahihi anayekustahili atakuja. Vaa ujasiri, huu ni wakati wa mwanzo mpya."





