Jurgen Klopp akubali kuwa kocha wa Ujerumani.
Joyce Shedrack
July 3, 2026
Share :
Kocha wa zamani Liverpool Jürgen Klopp amekubali kuwa kocha mkuu mpya wa timu ya taifa ya Ujerumani baada ya Julian Nagelsmann kufungishiwa virago.

Ripoti zinasema maelezo ya mwisho ya mkataba yanaendelea kukamilishwa kabla ya makubaliano rasmi, lakini Klopp tayari amekubali nafasi hiyo na ana hamu ya kuanza kazi hiyo.
Baada ya kufungua milango ya mazungumzo siku mbili zilizopita, Klopp sasa anatarajiwa kukamilisha vipengele vya mwisho vya makubaliano kabla ya kusaini mkataba wa kuchukua nafasi ya Julian Nagelsmann kama kocha mkuu wa Ujerumani.





