pmbet

Keneth akiri kuwauzia watu sumu ili wajiue

Eric Buyanza

May 30, 2026
Share :

Mwanamume mmoja amekiri mashtaka 14 ya kusaidia wengine kujiua nchini Canada baada ya kuuza sumu mtandaoni.

 

Kenneth Law, mwenye umri wa miaka 60, alikiri kosa hilo katika mahakama ya Ontario siku ya Ijumaa, kama sehemu ya makubaliano na waendesha mashtaka, ambao waliondoa mashtaka makubwa zaidi ya mauaji.
 

Mamlaka zilisema mpishi huyo wa zamani aliuza takriban vifurushi 1,200 vya sumu kwa wateja - ambao alikutana nao katika mijadala ya kujiua mtandaoni - katika nchi 40, takriban robo ya vifurushi hivyo vikitumwa Uingereza.
 

Mashtaka yote yanahusiana na waathiriwa wa Canada - lakini familia za waathiriwa wa Uingereza zimesema zimekasirika kwamba waendesha mashtaka wa Uingereza hawangemshtaki Law kuhusiana na vifo vya Waingereza 79, ambavyo mamlaka inasema vinahusiana na bidhaa alizouza eneo hilo.

 

Barua kutoka Huduma ya Mashtaka ya Kifalme, iliyoonekana na BBC, ilisema Law hatakabiliwa na mashtaka nchini Uingereza kwa sababu anaweza kupinga kupelekwa kwake baada ya kupatikana na hatia ya makosa kama hayo nchini Canada.

 

Law alikamatwa mnamo mwezi Mei 2023, kufuatia uchunguzi tata uliofanywa na takriban mashirika 11 ya kutekeleza sheria na kuwahusisha wachunguzi kutoka takriban nchi kumi na mbili, ikiwa ni pamoja na Uingereza, Italia na Marekani.
 

Kukamatwa kwake kulikuja wiki moja baada ya uchunguzi wa Times kudai alikuwa akiwauzia vijana sumu, baada ya mwandishi wa habari kujifanya mteja na kuzungumza na Law moja kwa moja.
 

Inasemekana Law alimshauri mwandishi wa habari jinsi ya kutumia bidhaa zake ili "kuhakikisha anakufa".
 

Makachero wa Canada waliiambia BBC mnamo 2023 kwamba Law aliendesha tovuti nyingi zinazotoa vifaa na sumu ili kuwasaidia watu kujiua.

 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet