Kenya yakumbwa na Ukame, waagiza maziwa Uganda
Sisti Herman
September 7, 2026
Share :

Kenya imesema inaagiza maziwa kutoka Uganda huku uhaba wa bidhaa hiyo nchini ukiendelea. Waziri wa Biashara, Uwekezaji na Viwanda, Lee Kinyanjui, amethibitisha hilo.
Waziri alitaja sababu ya uhaba wa maziwa unaoendelea nchini kuwa umetokana na kipindi kirefu cha ukame kilichowaathiri wakulima na kuvuruga uzalishaji wa maziwa katika maeneo kadhaa, na kuwahakikishia wakulima kuwa msaada wa serikali unakuja, huku kukiwa na juhudi mpya za kuisaidia nchi kufikia hatua ya kujitosheleza kwa uzalishaji wa maziwa.
Uganda imekuwa mmoja wa wadau wakubwa wa sekta ya maziwa katika eneo hili, ikizalisha takriban lita bilioni 5.3 hadi 5.4 za maziwa kila mwaka—kiasi kinachozidi mahitaji ya matumizi ya nchi hiyo yenyewe.





