pmbet

Kijana aenda jela kwa kutaka kuiba gari la polisi

Eric Buyanza

July 22, 2026
Share :

Mahakama nchini Ghana imemhukumu kifungo cha mwezi mmoja jela kijana mwenye umri wa miaka 26 baada ya kupatikana na hatia ya kujaribu kuiba gari la polisi.

 

Ebenezer Frimpong alikamatwa baada ya kuingia kwenye gari la polisi lenye ulinzi maalumu na kuondoka nalo, wakati dereva wake alipokuwa ameshuka kununua dawa katika duka la dawa mwezi Aprili mwaka huu.

 

Kwa mujibu wa dereva wa gari hilo, Joshua Denkyi, tukio hilo lilitokea alipokuwa ameegesha gari njiani ili kununua dawa.

Frimpong alikamatwa baada ya polisi kumfukuza alipokuwa akijaribu kutoroka na gari hilo.

 

Kabla ya kutoa hukumu, mahakama iliamuru afanyiwe uchunguzi wa afya ya akili ili kuthibitisha kuwa alikuwa na utimamu wa akili.

Baada ya kukiri kosa, jaji alimhukumu kifungo cha mwezi mmoja jela, akieleza kuwa adhabu hiyo imepunguzwa kwa sababu mshtakiwa alikiri kosa mapema na hakupoteza muda wa mahakama.

 

Source: BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet