pmbet

Kim Jong Un apiga marufuku watu kujiua nchini kwake

Eric Buyanza

December 12, 2025
Share :

Kiongozi mtata wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un amepiga marufuku watu kujiua nchini humo huku akikiita kitendo hicho “uhaini dhidi ya ujamaa.”
 

Agizo hilo jipya linakuja wakati huu ambao nchi hiyo inakabiliwa ongezeko kubwa la watu kujiua jambo ambalo halijawahi kutokea tangu kuanza kwa taifa hilo.

 

Hata hivyo inaelezwa kuwa ongezeko hilo linachangiwa na kuongezeka kwa hali ngumu ya maisha, njaa iliyoenea katika maeneo mengi ya vijijini, na kuongezeka kwa hali ya kutokuwa na matumaini miongoni mwa raia wa kawaida.

 

Chini ya sheria hiyo mpya, maafisa wa eneo sasa wanawajibika moja kwa moja kwa kila tukio la kujiua katika eneo lao.

Ikiwa mkazi atajiua, afisa anayesimamia eneo hilo atachunguzwa, kuadhibiwa au kupoteza kazi yake.

 

Hii imesababisha ufuatiliaji mkali kwa kaya zinazochukuliwa kuwa "hatarini" na kuongezeka kwa shinikizo kwa familia kutoa ripoti ikiwa wanaona dalili zozote za mwanafamilia kutaka kujitoa uhai.

 

Familia za wale wanaojaribu kujiua pia zinaweza kukabiliwa na adhabu ya pamoja.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet