pmbet

Kim Jong Un awasifia wanajeshi 'waliojiua' kuepuka kukamatwa

Eric Buyanza

April 29, 2026
Share :

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un amewapongeza wanajeshi wa wa nchi hiyo waliojitoa uhai kwa kujilipua wakati wakiipigania Urusi dhidi ya Ukraine, na kuthibitisha sera inayoshukiwa kwa muda mrefu kwenye uwanja wa vita.

 

Katika hotuba yake wiki hii, kiongozi huyo wa Korea Kaskazini alisema wale ambao "waliamua kujilipua bila kusita, walijitoa mhanga, ili kulinda heshima kubwa" ya nchi yetu ni "mashujaa".

 

Korea Kusini inakadiria kuwa takribani raia 15,000 wa Korea Kaskazini wametumwa kuisaidia Urusi kurejesha sehemu za magharibi mwa Kursk, na zaidi ya 6,000 wameuawa kufikia sasa.
 

Pyongyang na Moscow hazijathibitisha idadi hiyo ya vifo.

Mashirika ya kijasusi na walioasi wamesema wanajeshi hao walikuwa chini ya amri ya Pyongyang kujiua badala ya kuchukuliwa mateka na Ukraine.

 

"Walijitolea bila kutarajia fidia, wala kutarajia malipo... Hii [ndiyo] ufafanuzi wa uaminifu wa jeshi letu," Kim alisema mjini Pyongyang siku ya Jumatatu alipokuwa akizindua sanamu ya kumbukumbu ya wanajeshi waliofariki, vyombo vya habari vya serikali KCNA viliripoti.
 

Waziri wa Ulinzi wa Urusi Andrey Belousov na spika wa bunge la Urusi Vyacheslav Volodin ni miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo.

 

Huko Korea Kaskazini, wanajeshi wanafundishwa kuwa kukamatwa vitani ni kitendo cha uhaini.

 

Mapema mwaka huu, shirika la utangazaji la Korea Kusini MBC lilirusha hewani kipindi kilichowaangazia wafungwa wawili wa kivita wa Korea Kaskazini nchini Ukraine, mmoja wao alisema kwamba anajuta kwa nini hakujitoa uhai.
 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet