Kinara wa mabao Simba Queens apewa mkono wa kwaheri.
Joyce Shedrack
July 15, 2025
Share :
Klabu ya Simba imetangaza kuachana na mshambuliaji wake kinara raia wa Kenya Jentrix Shikangwa.
Mshambuliaji huyo anakuwa ni mchezaji wa 13 kuachana na wekundu wa msimbazi katika dirisha hili huku akiwa miongoni mwa wachezaji waliofanya vizuri msimu uliopita.
Shikangwa alimaliza msimu akiwa na magoli 24 huku akiwa ndiye mfungaji kinara kwa @simbaqueensctz akimaliza nafasi ya pili nyuma ya mfungaji bora wa ligi Stumai Abdallah wa JKT Queens aliyemaliza akiwa na magoli 28.