pmbet

Kiongizi wa upinzani Zambia ashtakiwa kwa uhaini

Sisti Herman

August 31, 2026
Share :

 

Mawakala wa kiongozi wa upinzani nchini Zambia, Brian Mundubile, wamethibitisha kuwa mteja wao amefikishwa mahakamani na kushtakiwa kwa kosa la uhaini, wakati mvutano wa kisiasa ukiendelea kushika kasi nchini humo. Wakili wake, Milner Katolo, amesema Mundubile yuko tayari kujitetea dhidi ya mashtaka hayo, huku akithibitisha taarifa hizo Jumamosi jioni katika mahojiano na Zambian Eye.

Mundubile alikamatwa Alhamisi kufuatia operesheni iliyofanywa na mamlaka, baada ya awali kujificha kufuatia hatua zilizokuwa zimechukuliwa dhidi yake. Kiongozi huyo wa upinzani alikuwa miongoni mwa walioshindwa katika uchaguzi wa hivi karibuni wa urais nchini Zambia, ambapo Rais Hakainde Hichilema alitangazwa mshindi na kupata muhula wa pili madarakani.

Mzozo huo wa kisiasa umeendelea kuongeza presha nchini Zambia, huku mamlaka zikikituhumu chama cha Mundubile, NRPUP, kwa kupanga uasi wa kutumia silaha, madai ambayo chama hicho kimekanusha na kuyaita tuhuma zinazotolewa dhidi yake. Kesi ya Mundubile sasa inatarajiwa kuendelea mahakamani, huku hatua za mahakama zikitoa mwelekeo wa namna mvutano huo wa kisiasa utakavyoendelea.
 

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet