Kiongozi wa wanajihadi Oumar Kéréna, auawa kwa 'Droni' ya jeshi
Eric Buyanza
June 15, 2026
Share :
Jeshi nchini Mali limedai kuhusika katika kumuangamiza kiongozi wa wanajihadi aliyekuwa akisakwa kwa muda mrefu anayetambuliwa kwa jina la Oumar Kéréna.
Jeshi hilo limesema lilimuua kiongozi huyo katika shambulio la ndege isiyo na rubani mnamo Juni 3 karibu na mji wa Djenné.
Oumar Kéréna anatajwa kuwa kamanda muhimu wa Jama'at Nusrat al-Islam wal-Muslimin (JNIM), kundi linalodaiwa kuwa na uhusiano na Al Qaeda.






