Kiungo wa Brazil asimulia Man United ilivyomkaushia dakika za mwisho
Sisti Herman
August 23, 2026
Share :

Kiungo wa Brazil Éderson amevunja ukimya kuhusu uhamisho wake ulioshindikana kwenda Manchester United na kusisitiza kuwa bado haelewi kilichotokea.
Kiungo huyo wa Atalanta amefichua kuwa vipimo vyake vya afya vilikwenda vizuri kabisa na kukiri kuwa "hana wazo" lolote kuhusu sababu iliyofanya uhamisho huo kufeli hatimaye.
Pia, Éderson aliweka wazi kuwa alikuwa na ofa nyingine na angeweza kujiunga na klabu nyingine ya Ligi Kuu ya Uingereza.





