Kocha wa zamani wa Yanga apigwa chini Kaizer Chiefs.
Joyce Shedrack
May 26, 2026
Share :
Klabu ya Kaizer Chiefs imeripotiwa kuamua kuachana na makocha wake, Cedric Kaze (BURUNDI) na Khalil Ben Youssef (TUNISIA),baada ya mikataba yao kuisha.

Kaze aliyewahi kuifundisha Yanga, na Khalil Ben Youssef, waliiongoza Amakhosi kumaliza katika nafasi ya tatu katika msimu wa 2025/26 wa Ligi Kuu ya Afrika Kusini, ikiwa ni mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka 6, na klabu hiyo kupata nafasi ya kushiriki Kombe la shirikisho msimu ujao.
Kulingana na FARPost, Chiefs wameamua kukata uhusiano na Kaze na Ben Youssef , ambao walipandishwa cheo kutoka kuwa wasaidizi wa Nasreddine Nabi, hadi makocha wenza hadi mwisho wa msimu uliomalizika hivi karibuni, wakati bosi wao alipoondoka Septemba mwaka uliopita.





