Kondo la nyuma la wamama wanaojifungua lageuzwa gesi ya kupikia
Eric Buyanza
June 24, 2024
Share :
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma imepongezwa kwa ubunifu wa kutumia kondo la nyuma la akinamama waliojifungua kwa ajili ya kuzalisha gesi ya kupikia na matumizi mengine ya hospitalini.
“Nawapongeza sana watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma kwa kutumia kondo la nyuma la mama aliyejifungua na kuliweka kwenye utaratibu maalum kwenye chemba maalum ambalo mwisho wa siku inabadilika kuwa gesi ya kupikia katika mahitaji ya hospitali”
“Leo kondo la nyuma la akinamama wanaojifungua siyo changamoto ya kutuumiza kichwa tutupe wapi? leo tunatamani yatoke mengi ili kuweza kuzalisha gesi zaidi kwa matumizi ya hospitali, hongereni sana”, amesema Dkt. Mollel.