"Kusema hapana kwa Real Madrid haikuwa rahisi"-Rodri.
Joyce Shedrack
September 15, 2026
Share :
Kiungo wa Manchester City Rodri amefichua kuwa miongoni mwa maamuzi magumu aliyowahi kuyafanya ni kuikataa Real Madrid licha ya kumthamini wakati wa mazungumzo ya kutaka kumsajili.

“Kusema hapana kwa Real Madrid haikuwa rahisi, pia kwa sababu walinitendea vizuri sana. Walikuwa na heshima kubwa kwangu wakati wa mazungumzo,”
Nyota huyo wa Hispania alieleza kuwa alilazimika kuzingatia mambo mengi kabla ya kufanya uamuzi, kwa kuwa alikuwa akichagua kati ya klabu mbili kubwa duniani.
“Nilipaswa kuzingatia mambo mengi na kufanya uamuzi muhimu sana kati ya klabu mbili bora zaidi duniani. Haikuwa rahisi,” Amesema Rodri.
Rodri pia amefichua kuwa kocha maarufu José Mourinho aliwahi kumpigia simu moja kwa moja na kueleza wazi nia yake ya kumtaka ajiunge na timu yake.
“José Mourinho alinipigia simu na kueleza wazi kwamba alitaka nijiunge na klabu hiyo. Aliniambia kile nilichoweza kuleta kwenye timu,” Rodri alisema.





