pmbet

Kusoma magazeti kwa mbwembwe ni ubunifu - Nape

Eric Buyanza

February 15, 2024
Share :

Waziri wa Habari na Mawasiliano, Mhe. Nape Nnauye, ameielekeza Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA, kuruhusu ubunifu kwenye tasnia ya Habari.
 

Maelekezo hayo yamefuata siku moja baada ya Mamlaka hiyo kuzuia usomaji wa magazeti kwa mbembwe, ambapo amebainisha kuwa staili mbalimbali za usomaji magazeti zimeongeza mvuto kwenye usomaji wa magazeti, hivyo jambo hilo ni la kutiwa moyo na sio kuzuiliwa.
 

Mhe. @napennauye ametoa maelekezo hayo kupitia mtandao wa X (zamani Twitter), ambapo pia ameitaka Mamlaka hiyo, kujenga utamaduni wa kuzungumza kabla ya kuagiza.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet