Kwanini mashabiki wa Simba wanafurahia Fadlu kutimuliwa?.
Joyce Shedrack
June 12, 2026
Share :
Usiku wa jana klabu ya RajaCasablanca ya Morocco ilithibitisha kumfuta kazi aliyekuwa kocha mkuu wa timu yao Fadlu Davids kufuatia mwenendo mbaya wa matokeo ya timu hiyo.

Fadlu ambaye alijiunga na Raja akitokea klabu ya Simba Septemba mwaka jana aliiacha Simba katika nyakati ambazo walimuhitaji zaidi baada ya kuwekewa mezani dau nono na Raja AC.
Baada ya kupewa mkono wa kwaheri katika klabu hiyo inayoshika nafasi ya tano kwenye ligi kuu ya Morocco mashabiki wa Simba wameonekana kufurahishwa sana na taarifa hizo wengine wakiweka wazi kuwa aliwaacha kwenye nyakati ambazo walimuhitaji zaidi.
Unadhani Wanasimba wapo sahihi kufurahia au ndo malipo ni hapa hapa duniani?.





