pmbet

Liverpool kumsajili Araujo wa Barcelona kwa mkopo

Eric Buyanza

August 8, 2026
Share :

Liverpool iko katika hatua za mwisho za kumsajili beki wa Uruguay, Ronald Araujo, kwa mkopo wa msimu mmoja kutoka Barcelona.
 

Makubaliano hayo yanajumuisha kipengele cha kumnunua moja kwa moja Araujo, ambaye anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya siku ya Jumapili.

 

Beki huyo wa kati mwenye umri wa miaka 27 ameisaidia Barca kutwaa taji la La Liga katika misimu mitatu kati ya minne iliyopita, na alimaliza msimu uliopita akiwa nahodha wa klabu hiyo.

 

Araujo ana mkataba unaoendelea hadi mwaka 2031 lakini alicheza mechi 11 pekee kama mchezaji wa kuanza katika ligi msimu uliopita, huku Gerard Martin na Pau Cubarsi wakionekana kuwa chaguo la kwanza katika safu ya ulinzi ya kati.

 

Tangu ajiunge na Barca akitokea klabu ya Boston River ya Uruguay mwaka 2018, Araujo ameichezea klabu hiyo kubwa ya Uhispania zaidi ya mara 200.

 

Liverpool ilikuwa ikitafuta kuimarisha safu yake ya ulinzi baada ya Ibrahima Konate kuondoka klabu hiyo na kujiunga na Real Madrid kwa uhamisho huru.
 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet