Mahakama kutoa uamuzi kuhusu ombi la Marasta kutumia Bangi katika ibada
Eric Buyanza
July 15, 2026
Share :

Dini inayotambulika lakini ni ibada iliyokatazwa: hiki ndicho kitendawili ambacho Mahakama Kuu ya Kenya inatarajia kushughulikia leo Julai 15, 2026.
Majaji wataamua kama wafuasi wa harakati za Marastafari wanaweza kufaidika na msamaha wa kidini unaowaruhusu kutumia bangi katika ibada zao. Uamuzi ambao unaweza kufafanua upya mipaka ya uhuru wa kidini nchini Keanya.
Nchini Kenya, kukamatwa na bangi kunaweza kusababisha kifungo cha hadi miaka 10 jela. Hata hivyo, kwa Marastafari, marufuku hii ni sawa na kuharamisha moja ya mila kuu za dini yao.
Jumuiya ya Rastafari ya Kenya haitoi wito wa kuhalalishwa kwa jumla kwa bangi. Inaomba msamaha kwa wafuasi wake, ikisema kwamba Katiba inalinda uhuru wao wa kuabudu kama kwa dini zingine.
"Ikiwa dini zingine zinaruhusiwa kutekeleza imani yao kama zinavyoona inafaa na desturi zao zinaheshimiwa, basi Warastafari lazima pia waheshimiwe," anasema Duncan Okatch, wakili katika Mahakama Kuu ya Kenya.
Kulingana naye, hoja nzima ya kisheria inategemea asili ya bangi katika imani ya Marastafari: "Kwao, bangi ni takatifu. Ni kama ushirika mtakatifu katika dini ya Katoliki. Zoezi hili linakuza kutafakari na kutafakari kiroho. Kwa hivyo linapaswa kulindwa." "
Walalamikaji wanategemea hasa Katiba ya 2010, ambayo inahakikisha uhuru wa dini na inakataza ubaguzi unaotokana na imani. Pia wanatumia Mkataba wa Afrika kuhusu Haki za Binadamu na Watu na Azimio la Haki za Binadamu la Ulimwengu. Katika ombi lao, wanadai kwamba hawatafuti haki mpya, bali tu kwamba “haki ambazo Katiba tayari inahakikishia dini zote pia zinawahusu na wao.”
“Mimea takatifu”
Vita hivi vya kisheria si vipya. Mnamo mwaka 2019, Mahakama Kuu ilikuwa tayari imetoa uamuzi wa kuipendelea familia ya Rastafari baada ya kufukuzwa shule kwa mwanafunzi aliyekuwa na nywele za rasta. Mahakama iliamua kwamba uamuzi huu ulikiuka uhuru wao wa dini, hivyo kutambua Urastafari kama dini inayolindwa na Katiba ya Kenya.
Rastafari (au Rastafarianism) ni vuguvugu la kidini na kitamaduni liloanzishwa nchini Jamaika miaka ya 1930. Vuguvugu hili huamini kuwa Mungu (wanaemwita Jah) yuko ndani ya kila mwanadamu.
RFI





