Majeruhi yamuondoa Mbeumo kambi ya Timu ya Taifa.
Joyce Shedrack
March 25, 2026
Share :
Mmoja wa nyota wa Kiafrika wa Manchester United Bryan Mbeumo atakuwa nje ya uwanja wakati wa mapumziko yajayo ya kimataifa kufuatia sare ya 2-2 ya Red Devil dhidi ya Bournemouth kwenye Ligi kuu ya Uingereza, Ijumaa iliyopita.
Wababe hao wa Uingereza wanajivunia safu kubwa ya nyota wa Afrika kwa sasa, ambao ni kupitia mastaa kama Amad Diallo, Noussair Mazraoui na Bryan Mbeumo.
Hata hivyo, hivi majuzi klabu hiyo ilithibitisha kwamba Mbeumo alijiondoa katika mechi za kirafiki za Cameroon dhidi ya Australia na China mwezi huu kama ‘tahadhari’.
Akijivunia mabao tisa na asisti tatu katika mechi 26 za Ligi Kuu msimu huu, Mbeumo alitolewa dakika ya 71 dhidi ya Cherries baada ya kuumia.





