MAJONZI OLD TRAFFORD: Carrick atokwa na machozi kisa kipigo
Eric Buyanza
September 17, 2026
Share :
Kocha mkuu wa Manchester United, Michael Carrick, ameshindwa kuzuia hisia zake na kutokwa na machozi mbele ya waandishi wa habari, kufuatia kipigo cha aibu cha mabao 3-2 dhidi ya Brighton, ambacho kimeiondoa timu hiyo kwenye michuano ya Carabao Cup.
Katika mkutano na waandishi wa habari Carrick alionekana kuwa na macho nyevunyevu, akishindwa kupata maneno ya kusema huku sauti yake ikitetemeka kwa mshtuko.
United walipoteza mchezo huo wa raundi ya tatu huko Old Trafford jana usiku, licha ya kuwa mbele kwa mabao 2-0 ndani ya dakika 10 za kwanza za mchezo kupitia kwa Marcus Rashford na Amad Diallo.






