Man United yamnyatia Ederson, kiungo mbrazil kutoka Serie A
Eric Buyanza
May 23, 2026
Share :
Manchester United wako kwenye mazungumzo ya kumsajili kiungo mbrazil Ederson wa klabu ya Atalanta ya Serie A.
Ederson anasemekana kushinikiza kuondoka Atalanta, na Mashetani Wekundu wanajadili mkataba wa miaka mitano huku kukiwa na ada ya euro milioni 45-50 kwa mchezaji huyo.






