pmbet

Marekani imetumia karibu akiba yake yote ya makombora nchini Iran

Eric Buyanza

August 5, 2026
Share :

Vyanzo viwili vimeiambia CBS News - mshirika wa BBC nchini Marekani - kwamba Marekani imetumia karibu akiba yake yote ya dunia nzima ya makombora ya masafa marefu yenye usahihi wa hali ya juu wakati wa vita dhidi ya Iran.

 

Kulingana na ripoti hii, Marekani imetumia karibu makombora yake yote ya aina ya *Army Tactical Missile System* (ATACMS) na makombora ya kushambulia kwa usahihi (*Precision Strike Missiles*) katika Operesheni Epic Fury.

 

Awali, Reuters iliripoti kuwa Marekani ilikuwa imetumia "karibu makombora yote" ya masafa marefu yenye usahihi wa hali ya juu katika operesheni hii.

 

CBS iliripoti hapo awali kuwa akiba ya Marekani ya makombora ya kuzuia mashambulizi (*interceptor missiles*) na makombora ya masafa marefu imepungua sana, na jambo hili limekuwa changamoto ya ndani kwa serikali.

 

Kulingana na ripoti hiyo, Marekani haiwezi kuendelea na mwenendo huu kwa kasi ileile iliyotumika kumaliza akiba ya silaha hizo mwanzoni mwa vita dhidi ya Iran.

 

Maafisa wa Marekani wamesema kuwa akiba ya makombora haya ni finyu, lakini suala la dharura zaidi ni idadi ya makombora ya kuzuia mashambulizi ya aina ya Patriot na THAAD, ambayo yanatumika kwa kasi kubwa kuliko uwezo wa viwanda vya ulinzi vya Marekani wa kuyazalisha.

 

Sean Parnell, msemaji mkuu wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon), alisema katika taarifa kwa CBS:
 

"Jeshi la Marekani ndilo jeshi lenye nguvu zaidi duniani na lina kila kitu kinachohitajika kutekeleza majukumu yake wakati wowote na mahali popote ambapo rais ataamua. Tumefanya operesheni kadhaa zilizofanikiwa katika maeneo mbalimbali huku tukihakikisha kuwa jeshi la Marekani lina akiba kubwa ya uwezo wa kulinda watu na maslahi ya taifa."

 

Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Pete Hegsett, hapo awali alitupilia mbali wasiwasi kuhusu kupungua kwa akiba ya silaha za Marekani. Aliambia CBS mnamo Julai 14:
 

"Hii ni habari ya kubuni ambayo vyombo vya habari vinataka kuisambaza. Hatimaye, akiba yetu iko katika hali nzuri na inaendelea kuimarika zaidi."

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet