pmbet

Marekani kuipa tena Ukraine mitambo ya kudungua makombora

Eric Buyanza

June 13, 2024
Share :

Tangazo la kutumwa kwa zana za kisasa za vita kwenda Ukraine, linakuja wakati huu ambapo rais wa  Ukraine Volodymyr Zelensky  amekua akitoa wito kwa mataifa washirika kuisaidia nchi yake vifaa zaidi vya ulinzi wa anga.

Zelensky amekuwa akitaka kuimarisha zaidi ulinzi wa anga la nchi hiyo haswa katika mji wa Kharkiv mashariki mwa Ukraine ambapo wanajeshi wa  Urusi  wameripotiwa kuzidisha kasi ya mashambulizi katika siku za karibuni.

Kwa mujibu wa gazeti la The New York Times, mitambo hiyo ya ulinzi wa angani kutoka Marekani kwa sasa ipo nchini  Poland ikiwa inaelekea Ukraine .

Washirika wengine wa  Ukraine  kutoka nchi za Magharibi akiwemo Kansela wa  Ujerumani Olaf Scholz , amekuwa akitoa wito wa kuisaidia Ukraine  kuimarisha zaidi ulinzi wake wa anga.

Ujerumani  tayari imeipa Ukraine  vifaa vitatu vya kudungua makombora angani.

RFI

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet