Marekani kupeleka maelfu ya wanajeshi mashariki ya kati
Eric Buyanza
March 25, 2026
Share :

Pentagon inatarajiwa kutuma maelfu ya wanajeshi kutoka kikosi maalumu cha Jeshi la Marekani, 82nd Airborne Division, kwenda Mashariki ya Kati, kwa mujibu wa Reuters. Hatua hiyo itaoongeza nguvu za kijeshi za Marekani huku Rais Donald Trump akizungumza kuhusu uwezekano wa makubaliano na Tehran kuhusu kumaliza vita.
Reuters iliripoti kwa mara ya kwanza tarehe 18 Machi kuwa utawala wa Trump ulikuwa unafikira kutuma majeshi zaidi, hatua ambayo ingeweza kupanua uwezekano wa kuhusisha operesheni ndani ya ardhi ya Iran.
Hatua kama hiyo ingeongeza hatari katika mzozo ambao tayari umeshaingia wiki ya nne na kuathiri masoko ya kimataifa. Maafisa hao, waliokuwa wakizungumza kwa sharti la kutotambulika, hawakutoa maelezo ya mahali ambapo wanajeshi hao watapelekwa au lini watapofika katika eneo hilo.
Kuhusu hili, msemaji wa White House, Anna Kelly alisema “Kama tulivyoeleza, Rais Trump daima ana chaguo zote za kijeshi kwenye mikononi yake,”.
Hadi sasa, hakuna uamuzi uliofanywa kutuma majeshi ndani ya Iran yenyewe, alisema chanzo kimoja, lakini hatua hii itaongeza uwezo wa Marekani kwa ajili ya operesheni zinazoweza kufanyika baadaye katika eneo hilo.





