pmbet

Marekani yalaani mawaziri 2 wa Israel kuwekewa vikwazo

Eric Buyanza

June 11, 2025
Share :

Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Marco Rubio amelaani hatua ya Uingereza, Norway, Australia, Canada na New Zealand kuwawekea vikwazo mawaziri wawili wa Israel wa mrengo wa kulia wenye misimamo mikali kutokana na mzozo wa Gaza.

Marco Rubio alilaani hatua hiyo, akiandika kwenye mtandao wa X: alisema "Vikwazo hivi haviendelezi juhudi zinazoongozwa na Marekani kufikia usitishaji vita, kuwarudisha mateka wote nyumbani, na kumaliza vita".
Aliyataka mataifa kubatilisha vikwazo hivyo, akiongeza kuwa Marekani "imesimama bega kwa bega na Israel."

Uingereza imewawekea vikwazo Waziri wa Fedha Smotrich na Waziri wa Usalama wa Kitaifa Ben-Gvir kwa sababu ya "kuchochea ghasia za itikadi kali na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu za Wapalestina".

Itamar Ben-Gvir na Bezalel Smotrich wote watapigwa marufuku kuingia Uingereza na mali yoyote nchini Uingereza itazuiwa kama sehemu ya hatua zilizotangazwa na waziri wa mambo ya nje.

Ni sehemu ya hatua ya pamoja na Australia, Norway, Canada na New Zealand iliyotangazwa Jumanne.

Ikijibu, Israel ilisema: "Inasikitisha kwamba wawakilishi waliochaguliwa na wanachama wa serikali wanachukuliwa hatua za aina hii."

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet