Mashabiki wa Afrika washangilia kipigo cha Afrika Kusini.
Joyce Shedrack
June 12, 2026
Share :
Baada ya mchezo wa kwanza wa Kombe la Dunia siku ya jana kati ya Mexico na Afrika Kusini maswali yamekuwa mengi kufuatia asilimia kubwa ya Waafrika kushangilia kipigo cha Timu ya Taifa ya Afrika Kusini.
![]()
Mashabiki wa Taifa la Nigeria wengi wao walijitokeza hadharani kabla ya mchezo wakiweka wazi kuwa wanaisapoti Mexico kwa sababu wakiisapoti Afrika Kusini Wananchi wao watasema wameingilia kazi zao.
Mchezo huo ulimalizika kwa kipigo cha mabao 2-0 walichokutana nacho Bafanabafana huku wakimaliza mchezo wakiwa wachezaji 9 baada ya nyota wao wawili kupewa kadi nyekundu.
Unadhani ni kwanini Waafrika wengi wamefurahia anguko la Timu ya Taifa ya Afrika Kusini usiku wa jana?





