pmbet

Mashambulizi yatarudi kwa nguvu na kiwango kikubwa zaidi - Trump

Eric Buyanza

May 7, 2026
Share :

Rais wa Marekani Donald Trump ameionya Iran kuwa itakabiliwa na mashambulizi mapya na makali zaidi endapo haitakubali mapendekezo ya amani yanayojadiliwa kati ya pande hizo mbili.

 

Kupitia ujumbe wake kwenye mtandao wa Truth Social, Trump alisema Marekani ilisimamisha kwa muda operesheni yake ya kijeshi katika Mlango wa Hormuz ili kutoa nafasi kwa juhudi za kidiplomasia, lakini akaonya kuwa mashambulizi yatarejea kwa “nguvu na kiwango kikubwa zaidi” ikiwa makubaliano hayatapatikana.
 

Kauli hiyo imekuja wakati Iran ikisema bado inatafakari pendekezo la Marekani lenye masuala 14, yanayolenga kumaliza vita pamoja na mvutano wa miezi miwili kuhusu udhibiti wa Mlango wa Hormuz.

 

Kwa mujibu wa ripoti mbalimbali za Marekani, pendekezo hilo linajumuisha kusitishwa kwa urutubishaji wa nyuklia wa Iran, kuondolewa kwa baadhi ya vikwazo na kurejeshwa kwa usafiri wa meli katika njia hiyo muhimu ya biashara ya mafuta duniani.
 

Hata hivyo, Trump amesema bado ni mapema kwa mazungumzo mapya ya moja kwa moja licha ya kile alichokiita “maendeleo makubwa” katika majadiliano ya siku za karibuni.
 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet