Mashindano ya Ngumi ya Ubingwa wa Wazi wa Taifa kuanza leo.
Joyce Shedrack
June 4, 2025
Share :
Mashindano ya Taifa ya Ubingwa wa Wazi - Dar es salaam 2025 (National Open Championship - Dar es salaam 2025) kuanza rasmi Leo Jumatano 04-06-2025 kwa mapambano ya awali ya mchujo (Preliminary stage) katika ukumbi maarufu wa ngumi chipukizi wa Manyara Park, Tandale.
Mashindano hayo ambayo ndio CHIMBUKO LA VIPAJI, yatashirikisha jumla ya mabondia 144 (8 Wanawake) kutoka vilabu vya mikoa ya Dar es salaam, Pwani, Mwanza, Dodoma, Morogoro, Kagera, Mwanza, Iringa na Njombe vikiwepo vya kutoka vyombo vya Ulinzi na Usalama ambao walifuzu zoezi la usajili (Sport entry check) na baadae upangaji rasmi wa ratiba ya mapambano (Official draw)
"Yes, ni msimu mpya wa Chimbuko la Vipaji 2025, na mwaka huu tumewafuata karibu kabisa na maeneo yenye vilabu vingi vya mtaani tuweza kuwapa fursa ya jukwaa kuonyesha vipaji vyao, mashindano haya pia yatatumika kuchagua vipaji vya kuviendeleza na kuwaongeza katika Timu ya Taifa bora ya mwaka 2024 ya Tuzo za Serikali za Baraza la Michezo la Taifa (BMT)" alisema Rais wa Shirikisho la Ngumi Tanzania (BFT) Ndg. Lukelo Willilo.
Mashindano haya yanayoendeshwa na Shirikisho la Ngumi Tanzania (BFT) ni ya pili ya kitaifa katika kalenda ya baada ya mashindano ya wanawake ya Samia yalitofanyika February, 2025.
Mashindano yataanza saa 8 mchana na hakutakua na viingilio katika hatua za awali na Fainali itakua siku ya Jumamosi 07-06-2025.
Hassan Juma (Nyekundu) kutoka Magereza akitangazwa mshindi dhidi ya Mohamed Mangochi kutoka Ngome (Blue) katika fainali ya uzani wa 57kg ya mashindano yaliyopita ya Ubingwa wa Wazi wa Taifa Dar es salaam 2024 yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo Cha Taaluma ya Polisi Dar es salaam. Mwamuzi Mohamed Kasilamatwe.