Mayele ageuka mfalme Pyramids akifunga goli baada ya miezi 4.
Joyce Shedrack
February 25, 2026
Share :
Mshambuliaji wa zamani wa Yanga Fiston Mayele amefunga goli baada ya kukaa siku 122 sawa na miezi 4 na siku 2 bila kufunga huku akiweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa Pyramids akifikisha magoli 50 ndani ya timu hiyo.

Mshambuliaji huyo wa DR Congo alitupia bao 1 katika ushindi wa kuvutia wa 3-1 wa Pyramids FC ugenini dhidi ya Ghazl El Mahallah usiku wa kumkia leo.





