pmbet

Mbappe aikimbia Nike, ajiunga na ON

Sisti Herman

September 20, 2026
Share :

 

Nyota Kylian Mbappé amebadili upande katika vita vya chapa za vifaa vya soka hasa viatu kutoka kukataa kuongeza mkataba mpya wenye thamani ya $17 Milioni (zaidi ya Tsh Bil. 44) za kampuni maarufu ya Nike kisha kujiunga na kampuni mpya ya ON ambapo anapata hisa katika kampuni hiyo

Inasemekana mkataba wake na Nike ulikuwa na thamani ya dola milioni 17 kwa mwaka. Sasa amejiunga na kampuni ya On (ambayo kwa sasa ina thamani ya takriban dola bilioni 9.2) kwa malipo ya pesa taslimu na hisa, akiungana na mwekezaji Roger Federer pamoja na Mkurugenzi wa Soka Thierry Henry.

Huo ni mkusanyiko wa watu wenye majina makubwa kwa ajili ya chapa ambayo viatu vyake vya soka havitaingia sokoni hadi mwaka 2027.

Majina hayo yatavutia mjadala. Lakini kuwashawishi wachezaji kuacha kutumia viatu vya aina ya Mercurial na Predator na kuhamia kwenye viatu hivi ndiyo changamoto halisi.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet