Mechi ya kuamua bingwa wa Kombe la Shirikisho kupigwa leo.
Joyce Shedrack
May 16, 2026
Share :
Mchezo wa marudiano wa Fainali ya Kombe la Shirikisho la CAF msimu wa 2025/2026 kati ya Zamalek na USM Alger unachezwa leo, Mei 16, 2026, katika Uwanja wa Kimataifa wa Cairo nchini Misri mjira ya saa 12 jioni kwa saa za Tanzania.
Mchezo wa kwanza uliopigwa nchini Algeria Mei 9, 2026, USM Alger ilishinda 1-0 kwa goli la mkwaju wa penati wa Ahmed Khaldi katika dakika ya 98 ya muda wa nyongeza.
Matokeo hayo yanaifanya Zamalek kuhitaji ushindi wa kuanzia mabao mawili kwa sifuri leo ili kutwaa ubingwa.





