Mechi ya Simba na Dodoma Jiji yaota mbawa
Sisti Herman
February 12, 2025
Share :
Mchezo wa Simba na Dodoma Jiji uliopangwa kufanyika Jumamosi Februari 15 umesogezwa mbele kutokana na kikosi cha Dodoma Jiji kupata ajali juzi.
Kikosi hicho kimepata ajali ya kudumbukia Mto Matandu Nangurukuru kilivyokuwa kinatokea Mkoani Lindi kucheza Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya klabu ya Namungo.
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara (TPLB) imethibitisha mchezo huo hauwezi kuchezwa kutokana na hali ya kikosi cha Dodoma Jiji.