Meneja: Zimbwe hadai Yanga, msipotoshwe
Sisti Herman
May 17, 2026
Share :

Baada ya mchezaji mwandamizi wa klabu ya Yanga, Mohammed Hussein Zimbwe kutoonekana uwanjani kwa wiki kadhaa sasa huku uvumi mtandaoni ukiibuka kuwa pengine ana mgogoro wa maslahi na timu hiyo, wakala wake Carlos Sylvester ameibuka na kusafisha hali ya hewa akibainisha kuwa mchezaji huyo yupo nje kwasababu ya majeraha na siyo kama inavyoripotiwa.
Kupitia Instagram yake Carlos ambaye ni Mkurungenzi wa Carl Pro Sports Agency ameandika hivi;
______
Napokea simu nyingi na sms Concerning Hii kitu
Mohammed Alipata majeraha kwenye mechi ya Ligi dhidi ya Mbeya City pale KMC Complex na club ilitoa hii statement, anaendelea na matibabu vizuri hajawa 100% Fit.
Mohammed Haidai club, Yanga paid 100% of His Signing-on Fees and all the agreed renumerarion.
He’s very Happy with the new Environment.
Thank you.
_____





