Miguel Gamondi awaponza kina Kibu wafungiwa kufanya usajili.
Joyce Shedrack
April 23, 2026
Share :
Kocha Mkuu wa Taifa Stars Miguel Gamondi amewatia matatani klabu ya Al-Nasr Benghazi ya Libya na kufanya wapigwe marufuku ya kusajili wachezaji na Shirikisho la Soka Duniani FIFA.

Adhabu hiyo imetokana na mgogoro na Miguel Gamondi, ambapo klabu imeamriwa kulipa fedha zinazodaiwa na hawataruhusiwa kusajili wachezaji wapya hadi deni hilo litakapolipwa.
Ikumbukwe Gamondi alijiunga na Al Nasr Februari 2025 na kuachana nao March mwaka huo huo kutokana na kudai mishahara na bonasi.





