Mkeyenge: Nini kimempata Pacome?
Sisti Herman
June 9, 2026
Share :

Anaandika mchambuzi wa michezo nchini @abdulmkeyenge1
________
Fundi wa balll Pacome Peodo Zouzoua sijui nini kimemtokea. Sio yule. Kuna namna majeraha yamemuathiri. Yupo katika timu na anapata nafasi ya kucheza kikosini, lakini sio hatoi kilicho bora.
Nimepitia majina ya wachezaji wenye Asist nyingi sijaona jina lake. Nimepitia majina ya wachezaji wenye mabao mengi sijaliona jina lake. Huwa inatokea katika maisha ya mpira. Sio siku zote unakuwa yule yule. Kuna kupanda na kushuka.
Pacome ameshuka kidogo, lakini bado haiondoi quality na kipaji kikubwa alichonacho. Waliomuita Profesa hawajakosea. Jamaa ni baller sana.
________
Yapi maoni yako?





