pmbet

Mkimtaka vunjeni benki

Sisti Herman

March 1, 2024
Share :

Rais wa klabu ya Napoli ya ligi kuu Italia De Laurentiis  amethibitisha kuwa kama klabu vigogo barani Ulaya watahitaji saini ya mshambuliaji wao kinara Victor Osimhen lazima watoboke mkwanja mrefu sana ili kuuvunja mkataba wake.

 

β€œKuna kipengele katika mkataba kinaruhusu mauzo ya Victor Osimhen japo ni kwa kiwango cha juu sana, Baadhi ya wachezaji hukaa Napoli kwa miaka mingi ... wengine wanasakwa na PSG, Arsenal, Man City au Chelsea, Ni ngumu kuwaweka wachezaji Napoli haswa wanapotakiwa na vilabu hivi tajiri vya Ulaya" alithibitisha Rais huyo.

 

Kifungu cha kununua mkataba wa Osimhen kitakuwa tayari kutumika kuanzia majira ya kiangazi 2024 na kinatajwa kuanzia kiasi cha Euro milioni 𝟏𝟐𝟎 hadi Euro milioni πŸπŸ‘πŸŽ.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet