Mo Dewji awahoji Simba Transformation imefikia wapi.
Joyce Shedrack
February 10, 2026
Share :
Mwekezaji na Rais wa heshima wa klabu ya @simbasctanzania Mohamed Dewji ameihoji klabu ya @simbasctanzania imefikia wapi kwenye mchakato wa mabadiliko ya uendashaji wa klabu ya Simba.
Mo Dewji ameuliza swali hilo kupitia ujumbe aliouandika kwenye jukwaa la kutoa maoni katika chapisho lililochapishwa na ukurasa wa Simba juu ya alichokizungumza Mwenyekiti wa klabu hiyo Murtaza Mangungu kwenye Mkutano wa Waandishi wa Habari siku ya leo.
Rais huyo wa heshima amenukuliwa alipoandika "Transformation imefikia wapi" kwenye chapisho hilo lililokuwa linahusu utolewaji wa kadi za uwanachama wa Simba.





