Mokwena apewa ofa Al Ittihad ya Libya
Sisti Herman
March 1, 2026
Share :

Aliyekuwa kocha wa Mamelodi Sundowns na kocha wa sasa wa MC Alger, Rulani Mokwena, anaripotiwa kuwarada za uhitajika na klabu kubwa ya Libya, Al Ittihad Tripoli, Kufuatia uamuzi wa klabu hiyo kuachana na kocha wa Tunisia, Khaled Ben Yahia, inasemekana kuwa mazungumzo na Mokwena yako katika hatua za juu.
Mkataba huo, ambao unakadiriwa kuwa na thamani ya takriban dola milioni 1.68 (zaidi ya shilingi bilioni 4.5 za Kitanzania), utamfanya kocha huyo wa Afrika Kusini mwenye umri wa miaka 39 kuondoka Algeria—ambako hivi karibuni alishinda taji la Super Cup—ili kuongoza klabu hiyo inayoongoza ligi ya Libya.
Ikiwa uhamisho huo utakamilika, Mokwena ataungana na winga wa Afrika Kusini, Thembinkosi Lorch, kwa mara ya nne katika maisha yake ya soka, huku Al Ittihad ikilenga kuimarisha uwezo wake kimataifa na mfumo wake wa mchezo.





