Morocco yakanusha taarifa za Walid Regragui kujiuzulu.
Joyce Shedrack
February 25, 2026
Share :
Shirikisho la Soka la Morocco limekanusha kwa mara nyingine taarifa zilizoibuka tena siku ya jana kuwa Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa Walid Regragui amejiudhulu wadhifa wake kabla ya Kombe la Dunia la FIFA la 2026.
Kupitia taarifa waliyoitoa kwenye tovuti rasmi, shirikisho hilo imesema Regragui, ambaye aliiongoza Simba hao wa Milima ya Barafu hadi nusu fainali ya kihistoria ya kombe la Dunia mwaka 2022, bado yuko chini ya mkataba huku maandalizi ya kombe la Dunia ya 2026 yakiendelea.





