Morocco yakanusha taarifa za Walid Regragui kutaka kujiuzulu.
Joyce Shedrack
February 7, 2026
Share :
Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini Morocco limekanusha taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii siku ya jana zilizoripoti kuwa kocha wa Timu ya Taifa ya Nchi yao Walid Regragui amewasilisha barua ya kutaka kujiuzulu nafasi hiyo.

"Shirikisho la Soka la Morocco linakanusha waziwazi kile ambacho kimesambazwa katika baadhi ya vyombo vya habari kuhusu kujiuzulu kwa kocha wa timu ya taifa, Bw. Walid Regragui, kutoka nafasi yake," tangazo hilo linasema.
Taarifa hii inathibitisha kwamba Regragui atakuwa kocha wa Morocco pia kwenye Kombe la Dunia mwaka 2026.





