Moto mkubwa wa msituni wazua taharuki Ufaransa na Hispania.
Joyce Shedrack
July 24, 2026
Share :
Maelfu ya watu wamehamishwa kutoka rasi ya Cap Ferret kusini-magharibi mwa Ufaransa baada ya mamlaka kuamuru eneo hilo lote liondolewe watu kutokana na moto mkubwa wa misitu unaoendelea kuenea.

Mamia ya wakazi na watalii walinusuriwa kwa kutumia boti, huku vikosi vya zimamoto vikipambana na moto ambao umeelezwa kuwa wa kiwango kikubwa sana (XXL).
Moto huo ulianza siku ya Jumanne na tayari zaidi ya hekta 10,000 za ardhi zimeteketea.
Wakati huo huo, nchini Hispania, serikali imetangaza hali ya dharura ya kitaifa baada ya moto wa misitu kuendelea kusambaa katika maeneo kadhaa karibu na mji mkuu wa Madrid.





