Mourinho ana hamu ya kuwa kocha ajaye wa Real Madrid
Eric Buyanza
May 2, 2026
Share :
Meneja wa Benfica, Jose Mourinho, ana nia ya kuwa kocha ajaye wa Real Madrid.
Hili limefichuliwa na nguli wa taarifa za uhamisho, Fabrizio Romano, kipindi hiki ambacho Madrid wana nia ya kumteua meneja mpya kuchukua mikoba ya Alvaro Arbeloa mwishoni mwa msimu huu.
Akizungumzia hilo Romano alisema, "Mourinho ana nia na yuko tayari kurejea Real Madrid.
"Ni hamu ya Jose Mourinho kurejea Real Madrid siku moja, kwa hivyo uwezekano wa kufanya hivyo msimu huu wa joto utakuwa jambo la kuvutia kwa 'The Special One' ."






