Msaidizi wa Tajiri Man United ajiweka pembeni na klabu
Sisti Herman
June 5, 2025
Share :
Sir Dave Brailsford, Mkurugenzi wa michezo wa kampuni ya INEOS inayoongozwa na tajiri wa Uingereza Sir Jim Ractliffe ambaye amewekeza hisa 25% za umiliki wa klabu ya Manchester United ameamua kukaa pembeni kujihusisha moja kwa moja na shughuli za klabu hiyo.
Wakati Brailsford atasalia kwenye bodi ya vilabu vya soka, ataelekeza nguvu zake katika jukumu lake pana kama mkurugenzi wa michezo huko INEOS.
Brailsford amekuwa na jukumu muhimu katika marekebisho ya United tangu Sir Jim Ratcliffe aliponunua hisa za chache katika klabu hiyo Desemba 2023.
Alikuwa kiongozi katika uboreshaji wa uwanja wa mazoezi wa United wa Carrington, ambao unatazamiwa kukamilika mwezi Agosti.
Hata hivyo, wakati uwepo wake umevutia ukosoaji katika baadhi ya maeneo, Brailsford inasalia kuwa karibu na Ratcliffe na atahusika kwa kiasi fulani United, lakini si katika kiwango sawa.
United wanaamini kuwa wana kundi dhabiti la uongozi wa kandanda, linaloongozwa na mtendaji mkuu Omar Berrada na pia mkurugenzi wa uajiri Christopher Vivell, mkurugenzi wa ufundi Jason Wilcox na mkurugenzi wa mazungumzo ya kandanda Matt Hargreaves.
Mkurugenzi wa zamani wa Utendaji wa mchezo wa Baiskeli wa Uingereza Brailsford alijiuzulu kama mkuu wa timu ya waendesha baiskeli INEOS Grenadiers baada ya Ratcliffe kupata hisa zake United.