pmbet

Msako mkali waja kwa wauza mafuta kwenye vidumu

Eric Buyanza

May 9, 2024
Share :

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji ( EWURA ) Kanda ya Magharibi, imetangaza kuanza msako mkali wa kuwakamata wafanyabiashara wanaouza mafuta ya petroli/dizeli kwenye vidumu na mapipa jambo ambalo linakiuka sheria na kuhatarisha maisha ya wananchi. 

Msako huo umetangazwa na Meneja wa EWURA  wa Kanda hiyo, Walter  Chirstopher,  wakati akiongea na waandishi wa habari ambapo alisema wafanyabiashara hao siku zao zinahesabika na wakikamatwa watafikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kukiuka sheria za mamlaka hiyo.

“Sheria  ya mafuta  ya mwaka  2015 kifungu  cha  131 inasema  mtu yoyote  haruhusiwi kuuza mafuta hayo bila kuwa na leseni  kutoka  EWURA,” amesema na kufafanua kuwa: “ Masharti ya EWURA mfanyabiashara anayotakiwa kuyatimiza ni kuwa na leseni na kujenga  kituo cha  mafuta."

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet