Muigizaji maarufu wa Nollywood, Alex Ekubo afariki dunia
Eric Buyanza
May 13, 2026
Share :
Muigizaji maarufu wa kiwanda cha filamu za kinigeria (Nollywood), Alex Ekubo, amefariki dunia jana Jumanne mchana.
Chanzo cha habari kutoka Nigeria kilisema muigizaji huyo alizidiwa ghafla na kukimbizwa Hospitali siku ya Jumatatu.
Taarifa zinasema Alex amekuwa akipambana na saratani ya figo toka mwaka 2024.






